Fid Q - Tajiri Yangu Feat Paul Clement (Official Video)
Fid Q Fid Q
161K subscribers
215,732 views
5K

 Published On Premiered Aug 13, 2020

#FidQ #TajiriYangu #PaulClement #SlideDigital

All praises due to the most high..
TAJIRI YANGU LYRICS:

Verse 1: ( Fid Q )

Lord.. ni ngumu kujua wewe uko wapi ila unajua nilipo/ ninaisaka haki kuipata ni bahati na kwa waganga siko/
Vyuma vikikaza tunatangatanga kuuchanga mshiko.. na mbanga zinakwaza madada wakidanga wanabamba vifo/

Na waliopinda wewe huwalinda na love/
Ka wale wajinga ambao hunipinga ninapouwinda wokovu/
Haunipi shida bila namna ya kuisolve/ wewe ndio mmiliki wa kila tiba na hauna iliyo mbovu /

Hauna iliyombovu.. unanipa uinchaji na power.. unaninyanyua juu/
Ni zaidi ya dawa.. sikuhitaji ninapougua tu/
Unaniweka sawa.. devil akitua hamchukui Q/
Una uwezo wa kunigawa au kuniumbua.. sio tu kuniumba mkuu/

ni rhumba tu ndio linaweka vumba juu na nakututesa kama mfungwa anayechungwa nakudundwa juu/

Wewe ndio BOSS ninayekuamini.. haututosi tukichomewa/ sio wale wanaowahi kazini ili wafoke tukichelewa...

Chorus ( Paul Clement )

Ewe Ewe.. tajiri yangu/
Wewe ndiwe kila kitu kwangu/
Ewe Ewe tajiri yangu/
Wewe ndiwe kila kitu kwangu
Ewe tajiri.. wa matajiri..
Ewe tajiri..Tajiri yangu/



Verse 2: ( Fid Q )

Mwanadamu amemtawala mwanadamu kwa kumuumiza/
Anakwapua mpaka asivyovihitaji bila kubakiza/
Hii inafanya nafsi yangu ikose subira/
Ikose usingizi, uoga., huzuni na hasira/

kwangu furaha ni kuwa na Mungu sio mlungura/
Na pia siku zote mla raha na uchungu hula/
Ninajua nilipotoka na ninajua wapi nilipo/ ispokuwa ni wewe pekee unajua lini nitafika mwisho/

cheo chako ni kirefu zaidi ya dunia... kipana zaidi ya bahari.. ulinzi mkali hakuna Askari anayefikia/
Ninamlaani shetani kiundani nipate kukujua mkuu/ ili nijihami na mtihani nisiache tusua Q/

Ninajua una huruma naomba nikibuma usinitose/ mwanadamu atazingua.. heshima sio utumwa kwa boss/ hawezi nunua uhai.. anajidai kwa lipi?/ na kwako sio tu akeshaye hata alalaye humpa riziki..

Chorus ( Paul Clement )

Ewe Ewe.. tajiri yangu/
Wewe ndiwe kila kitu kwangu/
Ewe Ewe tajiri yangu/
Wewe ndiwe kila kitu kwangu
Ewe tajiri.. wa matajiri..
Ewe tajiri..Tajiri yangu

Bridge ( Paul Clement )

Siwezi kuwa masikini sababu../
Anayenitunza ni tajiri.. ni Mungu/
Asiyeacha nigange njaa, nikosee furaha.. nikate tamaa/ eeh wee eeh wee tajiri yangu

Chorus ( Paul Clement )

Ewe Ewe.. tajiri yangu/
Wewe ndiwe kila kitu kwangu/
Ewe Ewe tajiri yangu/
Wewe ndiwe kila kitu kwangu
Ewe tajiri.. wa matajiri..
Ewe tajiri..Tajiri yangu

FID Q Songs OUT WORLDWIDE ON MAJOR DIGITAL STORES:

Written & Performed by Fid Q

Follow Fid Q on:
  / therealfidq  
  / fidq  

Channel Administered by Slide Digital
Instagram: www.instagram.com/slidedigitaltz

show more

Share/Embed